Pages

Tuesday, October 2, 2012


Afrika, ni bara la wanawake au wanaume?

Pamekuwa na mafanikio kadhaa kwa wanawake wa Afrika katika miezi kumi na miwili iliyopita,
kukiwepo tuzo mbili za Nobel, rais wa pili mwanamke na mwanamke wa kwanza kuwa mkuu wa Umoja wa Afrika. Kwa mjadala wa Afrika wa BBC, tunauliza iwapo wanawake wa Afrika wanaongezeka katika ngazi ya uongozi.
 
Ni rahisi kuamini kwamba wanawake wanaongezeka Afrika hususan mtu akizingatia kwamba Ellen Johnson Sirleaf ni rais wa Liberia na Joyce Banda wa Malawi.Kuanzia Julai mwaka 2012 Nkosazana Dhlamini-Zuma kutoka Afrika Kusini amekuwa kiongozi wa Umoja wa Afrika. Kwa kweli orodha ya wanawake wanaochukuwa nafasi za uongozi inaongezeka.
 
Hata hivyo maswali kadhaa yanapaswa kuulizwa kabla tuseme kuwa wanawake wanaongezeka kwenye ngazi ya uongozi au la.
Kwanza kabisa ni kipi chanzo cha ukandamizaji kwa wanawake? na je wanaweza kukabiliana na hili kwa wao kuwa marais wa nchi?
Ni kitu gani kinachojumuisha kuingia kwa wanawake uongozini Afrika. Wanawake wa Afrika ni wapi? Na hususan zaidi, wanawake hawa wanaochukua uongozi je ni wawakilishi wa wanawake Afrika?

Utafiti unaonyesha wazi kwamba kiini cha ukubwa wa mwanamume ni chanzo cha ukandamizaji wa wanawake wengi Afrika.
Ili wanawake waweze kuongezeka katika ngazi za uongozi, fikra ya kuwaona wanaume kuwa bora zaidi ni lazima ifutike.
Kutokana na uhusiano huu wa kijinsia, mtu huwaza je mwanamke kuchukuwa uongozi wa taifa hususan ikizingatiwa upendeleo uliopo wa jinsia moja katika taifa lenyewe, kutaleta mabadiliko?




Rasia wa Malawi Joyce Banda
 
 
kuna dhana kwamba hadi mtu atakapobadili mfumo unaompendelea mwanamume, mwanamke kujiunga katika uongozi wa taifa huishia kuwa mmoja wa wanaume na mfumo humlazimu kuwa kama mwanamume. Malawi

Na kwa hakika ili kudumu katika uongozi huo ni lazima awe na uwezo wa kutekeleza majukumu kama mwanamume na alihakikishie taifa kuwa ataendelea kuwatukuza wanaume.
Suala jingine muhimu kukumbuka ni kuwa hivi sasa ni nchi mbili pekee kati ya 54 Afrika zinaongozwa na wanawake.

Mizani hii iliyoegemea upande mmoja kwa wengine wanaitazama kuashiria kuongezeka kwa wanawake katika uongozi.
Kwa mujibu wa ripoti ya kongamano la uchumi duniani mwaka 2011 pengo la kijinsia linaashiria kuwa nchi kumi kati ya ishirini na moja zilizo na kiwango kikubwa cha ukosefu wa usawa wa kijinsia kati ya wanawake na wanaume zipo Afrika.
 

No comments:

Post a Comment